• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
MAANA YA KAZI

Maana ya Kazi 9. Maana ya neno ‘Kazi’

Utangulizi

Karibu tena ndugu msomaji katika mfululizo wa makala hizi za kujifunza juu ya maana ya kazi kwa lengo la kuboresha maisha yetu kila siku na kusaidia watu wengi ambao wanapaswa kufanya kazi ili kuingia kazini.

Katika mfululizo wa makala za tofauti ya kazi na ajira tumeanza kwa kuangalia maana ya neno kazi katika makala iliyotangulia. Leo tunazidi kuichambua maana hii ili kukujengea msingi muhimu wa kutofautisha kati ya neno ‘kazi’ na ‘ajira’ karibu sana.

Maana ya Kazi

Tuliona ya kuwa neno ‘work’ lina maana ya ‘an activity involving mental or physical effort done in order to achieve a purpose or result’. Kwa tafsiri isiyo rasmi tunaweza kusema kazi ni shughuli inayohusisha akili au nguvu za mwili kwa lengo la kufikia kusudi au kupata matokeo yaliyokusudiwa.

Kwa kuitazama tafsiri hii tunaweza kupata mambo yafuatayo ndani ya neno ‘kazi’

  • Kusudi au lengo; ili kazi iwepo ni lazima kuwe na kusudi au sababu ya mtu kufanya au kutaka kufanya kile anachofanya. Lazima mtu awe na sababu kwa nini anatumia akili yake au nguvu zake kufanya anachofanya.
  • Matumizi ya akili au nguvu; kazi inahusisha matumizi ya akili au nguvu au vyote kwa pamoja yaani akili na nguvu. Haitoshi tu kuweka lengo au kuwa na kusudi lazima hatua zichukuliwe kufanya kitu kwa kutumia akili na nguvu ili kupata matokeo yanayotarajiwa.
  • Matokeo; matokeo ni zao la kazi. Yapo matokeo ya aina nyingi inategemea kusudi la mtenda kazi alilokuwa nalo kabla hajawekeza akili na nguvu zake katika kazi husika. Mtu anaweza kupata matokeo ya furaha kama lengo ilikuwa kufurahi au kuona wengine wakisaidika kama lengo ilikuwa kutoa msaada kwa kazi yake au kupata fedha kama lengo la kazi ilikuwa fedha.

Hivyo mtu akisema anafanya kazi maana yake ana kusudi ndani yake ambalo analifikia kwa kuweka akili yake na nguvu zake kwenye matendo ili hatimaye apate matokeo aliyokusudia. Hii ndio maana halisi ya neno kazi. Hivyo mtu yeyote mwenye lengo au kusudi na kuwekeza muda wake akili yake na nguvu zake kuhakikisha anafikia lengo lake basi huyo ni mfanyakazi au mtenda kazi.

Nisisitize ya kuwa si lazima lengo la mtu huyo liwe kupata fedha bali anaweza kuwa anafanya anachofanya kwa malengo mengine kabisa labla kubadilisha maisha ya watu au kuleta furaha au kusaidia n.k

 Asiyetaka kufanya kazi na asile…’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
July 4, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-07-04 07:04:522020-07-04 07:04:57Maana ya Kazi 9. Maana ya neno ‘Kazi’
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.35. Spiritual Food: Nini maana ya uzima wa milele? Day.36. Spiritual Food: Je, unakijua chakula cha uzima?
Scroll to top