• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
MAANA YA KAZI

Maana ya Kazi 8. Unafanya Kazi au uko kwenye Ajira?

Utangulizi

Karibu tena ndugu msomaji katika mfululizo wa makala hizi za kujifunza juu ya maana ya kazi kwa lengo la kuboresha maisha yetu kila siku na kusaidia watu wengi ambao wanapaswa kufanya kazi ili kuingia kazini.

Watu wengi wanafahamu ya kuwa kazi ni sawa na ajira au mtu akiwa ameajiriwa ndio anafanyakazi. Ndio maana mtu anaweza kuitwa mfanyakazi au mwajiriwa. Maneno haya yote yanaweza kutumika kumaanisha dhana moja. Hatahivyo, ipo tofauti kubwa sana kati ya maneno haya mawili yaani ‘kazi’ na ‘ajira’. Kushindwa huku kutofautisha maana ya maneno haya kumewafanya watu wengi kufikiri kwa sababu wameajiriwa basi ni wafanyakazi na wale wafanyakazi kufikiri wao ni waajiriwa.

Ni muhimu sana katika maisha kwenye jambo lolote mtu ujue tafsiri sahihi kuhusiana na jambo husika. Kama ukifahamu tafsiri halisi ya neno ‘kazi’ na tafsiri ya neno ‘ajira’ inaweza kusaidia sana kubadili mfumo wako wa maisha. Katika mfululizo wa makala hizi za maana ya kazi tunakwenda kujifunza juu ya tafsiri ya maneno haya na tofauti zake ili kukusaidia kujua kilicho muhimu katika maisha yako na kuchukua hatua stahiki.

Maana ya Kazi

Ukisoma katika kamusi ya kiingereza neno kazi linatafsiriwa kama ‘work’. Kwenye kamusi ya kiingereza neno ‘work’ ikiwa na maana ya ‘an activity involving mental or physical effort done in order to achieve a purpose or result’. Kwa tafsiri isiyo rasmi tunaweza kusema kazi ni shughuli inayohusisha akili au nguvu za mwili kwa lengo la kufikia kusudi au kupata matokeo yaliyokusudiwa. Hii ina maana kuwa neno kazi linausisha uwezo wa mtu kutumia akili yake au nguvu zake katika kufanya jambo au shughuli ili kufanikisha lengo au kusudi au kupata matokeo anayotarajia.

Kwa mantiki ya tafsiri hii tu ya neno tunaona kazi si lazima ihusishe kupatikana kwa fedha ingawa fedha inaweza ikawa mojawapo ya matokeo ya kazi.

Endelea kufuatilia makala hizi tunapoifafanua zaidi maana ya ‘kazi’

 Asiyetaka kufanya kazi na asile…’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
July 3, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-07-03 01:10:192020-07-02 21:49:05Maana ya Kazi 8. Unafanya Kazi au uko kwenye Ajira?
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.34. Spiritual Food: Je, unaamini maneno ya Yesu Kristo? Day.35. Spiritual Food: Nini maana ya uzima wa milele?
Scroll to top