• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
KIPAJI CHANGU

Kipaji.7. Changamoto ya Kutonoa kipaji

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu katika mafunzo juu ya Kipawa/Vipawa katika ukurasa huu wa vipaji. Katika makala iliyopita tuliona changamoto ya Umri kumzuia mtu kutumia kipaji chake. Leo tunaangalia sababu nyingine ni Kutonoa kipaji

Sababu 4. Changamoto ya Kutonoa Kipaji

Tunafahamu ya kuwa kipaji ni zawadi ya bure ambayo mtu huzaliwa nayo. Kila mtu anacho kipaji iwe anakijua au hakijui lakini anacho kipaji. Unaweza kuvuka kihunzi cha kutokujua kipaji chako na ukapata kukifahamu mapema lakini bado ukakwamishwa na kutoweza kukitumia kipaji hicho kwa kutojizoeza kunoa kipaji chako.

Wengi wetu tunafuatilia sana juu ya wanamichezo hasa wa mpira wa miguu au kikapu au wakimbiaji mbalimbali. Tunawatazama watu hawa na kuwaona ni wa tofauti sana na sisi kwa sababu ya uwezo na ujuzi wanaoonesha katika vipaji vyao. Kitu muhimu ambacho tunashindwa kukifuatilia ni kuwa wana utaratibu wa kunoa vipaji vyao katika maisha yao ya kila siku. Ndio maana hata mchezaji awe na kipaji kiasi gani ni lazima afanye mazoezi ili kupata nafasi ya kucheza kwenye timu.

Mazoezi au kunoa kipaji ndio siri ya kujitofautisha na watu wengine wenye kipaji cha aina yako. Kama wewe ni mwimbaji mzuri hatutaweza kukujua kati ya waimbaji wengi kama huna mazoezi ya kujitofautisha na wengine wengi. Kunoa kipaji ndio msingi wa kujitofautisha na wengine wenye kipaji kama chako.

Unaweza ukawa na sifa nzuri kama mchoraji au mwandishi au mwigizaji lakini kama hutuoni namna unavyojinoa na kujifua kila siku basi utaishia kusema mimi mwenyewe naweza lakini wengine wenye kipaji kama chako wataonekana kwa sababu wanawekeza muda mwingi kunoa vipaji vyao.

Haitoshi tu kusema unacho kipaji hakikisha unaweka mpango mkakati wa kunoa kipaji chako kila siku ili kikutofautishe na wengine wengi wenye kipaji kama chako.

‘Kipaji changu, fursa yangu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
June 27, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-06-27 07:26:492020-06-27 07:30:15Kipaji.7. Changamoto ya Kutonoa kipaji
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.30. Spiritual Food: Acha Kunung’unika Day.31. Spiritual Food: Yesu ndiye Ufufuo
Scroll to top