• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.38. Spiritual Food: Unaweza kula lakini ukafa

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji ni siku nyingine tena tumepewa na Mungu kwa ajili ya kuendelea kujifunza zaidi misingi ya chakula cha kiroho ili kutuwezesha kufanya mapenzi yake na kumtumikia kwa furaha na upendo siku ya leo.

‘Baba zenu waliila mana jangwani wakafa’ Yn.6:49

Mambo ya kujifunza

  • Bwana Yesu anawakumbusha wayahudi juu ya historia ya baba zao walipotoka Misri na kuingia jangwani kwa safari ya Kanaani. Mojawapo ya muujiza mkubwa Mungu alioufanya katika safari hii ya miaka 40 ni kuhakikisha wana wa Israel wanapata chakula kila siku.

  • Mungu alimpa maagizo Musa kwa ajili ya wana wa Israel ya kuwa kila siku asubuhi kabla ya kuchwa watoke nje na kuokota chakula ambacho Mungu anawapatia na yakuwa siku ya 6 wataokota mara 2 zaidi ili siku ya 7 wasitoke kuokota. Maagizo haya waliyashika kwa takribani miaka 40. Lakini tunafahamu hatma ya wana wa Israel hawa hawakuingia Kanaani pamoja na kupata chakula kile wakati wa safari yao. Wengi walikufa jangwani. Ni watu 2 pekee ndio walioanza safari kutoka Misri na kufika Kanaani miongoni mwao yaani Yoshua na Kalebu. Soma zaidi Hes.14.

  • Hapa tunajifunza ya kuwa kipo chakula ambacho unaweza kupata lakini kisikupe uhakika wa maisha na kumaliza safari uliyokusudiwa. Haikuwa mpango wa Mungu kuwatoa Misri na wafie jangwani ila kwa sababu ya uasi wao na kutokumwamini Mungu ndivyo walishindwa kuingia Kanaani.

  • Hapa tunajifunza ya kuwa Mungu anaweza kukutoa katika utumwa kule Misri lakini sio ‘guarantee’ ya wewe au mimi kufika Kanaani kule Mungu alikokusudia. Si kwamba Mungu anashindwa kutufikisha bali itategemea imani yetu juu ya huyu Mungu. Wapo watakaofika lakini pia wapo watakaoshindwa kufika.

  • Tunaweza kupata ‘mana’ kwa ajili ya kutusaidia katika safari, je tutaendelea kumtegemea Mungu kila siku, tutakuwa na utii wa neno lake na maagizo yake kila siku? Hapa ndipo mtihani mkubwa upo kwa ajili yetu. Fikiria safari ya wana wa Israel ni  watu wawili tu walioweza kutoka mwanzo wa safari hadi mwisho kati ya wale waliokuwa na umri kuanzia miaka 20, wengi walioingia Kanaani ni wale waliozaliwa jangwani.

  • Yesu Kristo anatuonya ya kuwa baba zetu walikula mana lakini walikufa, je sisi tunataka kuwa hai na kufika mwisho wa safari yetu salama? Tuna kila sababu ya kumsikiliza kila hatua ya maisha yetu hata kama tutapitia mambo magumu.

MAOMBI LEO

Ndugu yangu ikiwa ndani yako unashuhudiwa bado huna uhakika wa maisha yako na kumjua Mungu ipasavyo, ujue unahitaji ufahamu huo kupitia uzima wa Mungu kuingia ndani yako. Karibu ufuatane nami katika kuomba maombi haya ili uzima wa Mungu ukae ndani yako sasa;

‘Ee Mungu Baba ninakushukuru kwa neno lako la uzima, asante kwa sadaka ya Mwana wako Yesu Kristo pale msalabani kwa ajili yangu. Bwana Yesu ninakiri udhaifu wangu na wasi wasi wangu wa kupotea milele endapo nitaondoka katika maisha haya. Ninaomba unisamehe dhambi zangu zote nilizofanya na hata kuondoa asili ya dhambi ndani yangu, unitakase kwa Damu yako takatifu. Ninaomba ufute jina langu katika kitabu cha hukumu na kuliandika katika kitabu cha uzima. Ninaomba uniokoe na kunifanya upya ndani yangu kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Uingie ndani yangu na kuniongoza tangu sasa na hata milele’ Amen.

Ikiwa umefanya sala hii kwa imani, Mungu kwa neema yake amekurehemu na kukusamehe kabisa, hata kama umefanya dhambi yeye ameisafisha na kuisahau. Unapaswa na wewe kujisamehe na kumfuata Yesu tangu sasa.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

 ‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
July 8, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-07-08 06:23:122020-07-08 06:23:19Day.38. Spiritual Food: Unaweza kula lakini ukafa
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.37. Spiritual Food: Nini maana ya Yesu kuwa chakula cha uzima? Day.39. Spiritual Food: Kula uishi
Scroll to top