• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.27. Spiritual Food: Mtazame Yesu sikuzote

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji ni siku nyingine tena tumepewa na Mungu kwa ajili ya kuendelea kujifunza zaidi misingi ya chakula cha kiroho ili kutuwezesha kufanya mapenzi yake na kumtumikia kwa furaha na upendo siku ya leo.

‘Kwa kuwa mapenzi ya Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho’ Yn.6:40

Mambo ya kujifunza

  • Andiko hili tunaona juu ya ahadi ya Bwana Yesu Kristo kwa ajili ya kila anayemwamini ya kuwa anapata uzima wa milele. Haya ni mapenzi ya Mungu Baba kwa kila mtoto wake ndani ya Kristo.

  • Tunaweza kuwa tumesikia watu wakituhubiria na kutuvutia kwao au kwa mambo au miujiza wanayofanya lakini hawatuelekezi kwa Yesu Kristo. Mwamini unapaswa kuwa na uhusiano wako binafsi na Yesu kwani hakuna mwanadamu atakayesimama kati yako na Mungu.

  • Tusiyumbishwe na sauti za watu hata katika dini au madhehebu tunayotumia kuabudu kwa kufuata watu bali tumfuate Yesu Kristo pekee.

  • Hatari kubwa ya kuwatazama watu ni pale wanapokutana na changamoto za majaribu basi mwamini naye huanguka kwa kuwa aliweka matumaini ya maisha yao kwa mtu ambaye si Kristo.

  • Swali muhimu kujiuliza mimi na wewe siku ya leo, Je ninapokutana na changamoto au shida yoyote ninamtazama nani? Ni wapi ninaanza kutafuta msaada? Maandiko yanatueleza amelaaniwa yule amtegemeaye mwanadamu na kumfanya kuwa kinga yake na moyoni amemwacha Bwana.
  • Uzima wa milele hatuupati kwa mtu wala hatufufuliwi kwa matakwa ya mtu bali kwa kigezo cha kumtazama Yesu kila siku na kumwamini katika mambo yote.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

 ‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
June 16, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-06-16 20:29:272020-06-16 20:29:35Day.27. Spiritual Food: Mtazame Yesu sikuzote
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.26. Spiritual Food: Ahadi ya Bwana Yesu kwa ajili yako Sehemu ya 7. Aina za Kazi
Scroll to top