• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.25. Spiritual Food: Je, unajua Yesu alikuja duniani kwa ajili yako?

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji ni siku nyingine tena tumepewa na Mungu kwa ajili ya kuendelea kujifunza zaidi misingi ya chakula cha kiroho ili kutuwezesha kufanya mapenzi yake na kumtumikia kwa furaha na upendo siku ya leo.

‘Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili nifanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka’ Yn.6:38

Mambo ya kujifunza

  • Andiko hili tunaona dhahiri ya kuwa Bwana Yesu alikuja duniani kutokana na agizo la Baba wa mbinguni na alikuja kutimiza kile alichotumwa na Baba wa mbinguni.

  • Wengi tunaifahamu historia ya mwanadamu pale Edeni jinsi wazazi wetu wa kwanza Adam na Hawa walipoasi kwa kufanya kile walichokatazwa na Mungu. Tangu wakati huo Mungu alikuwa anatekeleza hatua mbalimbali za ukombozi wa mwanadamu. Hatua hizi zilikuja kuhitimishwa kwa ujio wa Yesu Kristo katika mwili yaani Mungu mwenyewe.

  • Tangu wakati wa Yesu Kristo kufa na kufufuka hakuna wokovu wa mwanadamu yeyote isipokuwa kwa kupitia Yesu Kristo mwenyewe. Maandiko yanaeleza wazi kuwa Mungu ni mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja ambaye ni Yesu Kristo.

  • Kazi yote hii aliyoifanya Yesu Kristo pale msalabani ilitulenga mimi na wewe ili tuokolewe kutoka katika sheria ya dhambi na mauti na kuingia katika sheria ya Roho wa uzima.

  • Neno linasema ya kuwa Yesu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopotea. Sisi sote tunazaliwa katika hali ya dhambi haijalishi dini zetu au historia ya familia zetu kuhusiana na Mungu bali kila mmoja anahitaji kujenga uhusiano wake binafsi na Mungu.

  • Ni lazima ieleweke ya kuwa haitoshi tu kuzaliwa kwenye dini ukafikiri unao uhusiano na Mungu kutokana na kuwa ‘mkristo’. Paulo alizaliwa kwenye dini ya kiyahudi na akawa farisayo kweli kweli katika elimu ya dini lakini alipokutana na Yesu maisha yalibadilika. Nikodemo alikuwa mwalimu wa dini ya kiyahudi lakini Bwana Yesu alimpa shule ya kwamba mtu hawezi kuingia ufalme wa Mungu pasipo kuzaliwa mara ya pili.

  • Lazima ufahamu ya kuwa dini yoyote ile ni juhudi za mwanadamu kumtafuta Mungu lakini WOKOVU ni mpango wa Mungu kumtafuta mwanadamu. Chagua kukaa ndani ya mpango wa Mungu uwe salama.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

 ‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
June 12, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-06-12 06:02:222020-06-12 06:02:27Day.25. Spiritual Food: Je, unajua Yesu alikuja duniani kwa ajili yako?
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Kipaji.6 . Changamoto ya Umri AES.9. Changamoto za Mfumo rasmi wa Elimu – Ushindani usio na tija
Scroll to top