• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.24. Spiritual Food: Yesu awakubali wakosa

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji ni siku nyingine tena tumepewa na Mungu kwa ajili ya kuendelea kujifunza zaidi misingi ya chakula cha kiroho ili kutuwezesha kufanya mapenzi yake na kumtumikia kwa furaha na upendo siku ya leo.

‘Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe’ Yn.6:37

Mambo ya kujifunza

  • Sisi sote tunapelekwa kwa Bwana Yesu kwa mapenzi ya Mungu pekee na wala si kwa nguvu zetu au kutaka kwetu wenyewe. Wengine tumezaliwa na kukuta wazazi wetu katika imani ya kikristo. Tunaweza kufikiri kwa utashi wetu au urithi wa imani ya wazazi wetu tunaamini katika Kristo. Hii si kweli tunajaliwa kumjua Yesu kwa neema yake Mungu wetu.

  • Mtu unaweza kuzaliwa na wazazi ambao wameshika imani ya Kristo lakini wewe binafsi usiwe na mahusiano na Yesu Kristo. Jambo hili pia Bwana Yesu aliliona kwa kijana tajiri aliyeshika amri tangu utotoni, lakini alipoambiwa kuuza mali na kumfuata Yesu alihuzunika moyoni.
  • Mtu unaweza kuudhuria ubatizo, kipaimara, na ibada zote lakini bado ndani yako usiwe umejenga mahusiano binafsi na Mungu. Lazima tufahamu si kuzaliwa kwetu kwa mwili, au nafasi tulizonazo kwenye Kanisa au jamii bali neema ya Mungu anayotujalia kutukutanisha na Mwanawe wa pekee Yesu Kristo ndio inatupa kujenga uhusiano na Mungu siku kwa siku.

  • Bwana Yesu ameahidi ya kuwa kila amwendeaye hatomtupa nje kamwe. Inawezekana katika maisha yetu na kuenenda na Bwana tumekosea, tumeanguka kwa dhambi Fulani, kiasi ya kuwa hata wenyewe tunashindwa kujisamehe, Bwana Yesu anasema kila ajaye kwangu sitamtupa kamwe.

  • Tukiamini neno hili tusogee kwenye kiti chake cha rehema ili tupate neema wakati huu kuhuisha roho na nafsi zetu.

  • Tusikubali kukaa nje ya Bwana Yesu hata dakika moja zaidi ni hatari sana kwetu. Shetani asituhukumu kwamba hakuna msamaha kwetu, twende kwake kwa njia ya toba atatukubali.

Yesu awakubali

Wakosa, wahalifu,

Waambieni wa mbali,

Habari ya wokovu

Tangazeni kwa bidii,

Akubali wakosa,

Liwe neno dhahiri,

Akubali wakosa.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

 ‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
June 11, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-06-11 06:31:432020-06-11 06:31:49Day.24. Spiritual Food: Yesu awakubali wakosa
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Kipaji.5. Kutokutumia Kipaji Kipaji.6 . Changamoto ya Umri
Scroll to top