• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.21. Spiritual Food: Yesu Kristo ndiye chakula cha Uzima

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji. Ni siku nyingine tena tumepewa na Mungu kwa ajili ya kuendelea kujifunza zaidi misingi ya chakula cha kiroho ili kutuwezesha kufanya mapenzi yake na kumtumikia kwa furaha na upendo siku ya leo.

‘Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hatoona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe’ Yn.6:35

Mambo ya kujifunza

  • Hatimaye katika maneno haya tunaona Bwana Yesu akijitambulisha kwa Wayahudi kuwa Yeye ndiye Chakula cha uzima. Hili ni jambo jipya kwao kwa sababu hawakuwahi kusikia wala hawakutegemea kusikia. Mstahii huu hasa ndio kiini cha mazungumzo yote ya Yohana sura ya 6.

  • Muda wote wa mazungumzo walifikiri kipo aina ya chakula kama kile walichokula baba zao jangwani, lakini mwisho chakula hicho ni Yesu mwenyewe. Ujumbe huu pia ni kwa ajili yetu jinsi ya kumtazama Yesu katika sura na nafasi nyingine anayojifunua kama chakula cha uzima.

  • Watu wengi tunamfahamu Yesu kama mwokozi wetu, Bwana wetu au mponyaji wetu, lakini si wengi wanaifahamu sura hii ya Yesu kama chakula cha uzima. Yaani tukimjua Yesu kama chakula cha uzima na kuhakikisha tunakula kila siku chakula chake tunao uzima wetu wa sasa na hata baada ya maisha haya.

  • Ili kuona matokeo yoyote ya mambo ya kiroho suala la imani ni jambo la msingi sana. Kama hatuna tafsiri ya kwamba Yesu ni chakula cha uzima hatuwezi kupokea faida zinazotokana na Yesu kama chakula.

  • Tunapokea wokovu kwa kuamini juu ya kazi ya Yesu pale msalabani na msamaha wa dhambi tuliopata, lakini kuhusu mfumo wa maisha ya uzima ndani ya Yesu tunapaswa kuupokea kwa kuhakikisha tunaishi kwa chakula cha kiroho ambacho ni neno la Yesu kila siku.

  • Watu wengi pamoja na kuokoka kwa muda mrefu hawaoni maendeleo au kukua kiroho, sababu mojawapo kubwa ni kutokuwa na mfumo mzuri wa kupokea chakula cha kiroho kila siku.

  • Ukitaka kuona hatua zaidi katika maisha yako ya kiroho na kujenga uhusiano mzuri na Mungu kila siku, basi unapaswa ndani yako kubadili mtazamo na kuanza kutafuta kwanza chakula cha kiroho kitokacho kwa Yesu Kristo ambaye amejitambulisha kwetu kama chakula cha uzima.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

 ‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Je, una shida ya kusamehe au kushindwa kuomba msamaha?

Basi kama una changamoto ya suala zima la msamaha jiunge na mtandao wetu kwa kujisajili kisha tutakutumia zawadi ya BURE kabisa ya kitabu cha

‘Kwa nini Unalazimika kusamehe?

Kusamehe ni kwa faida yako kwanza

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
June 6, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-06-06 05:53:452020-06-06 05:53:58Day.21. Spiritual Food: Yesu Kristo ndiye chakula cha Uzima
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.20. Spiritual Food:Jenga hamu ya Chakula cha Kiroho kila siku AES.7. Changamoto za Mfumo rasmi wa Elimu – Ubaguzi
Scroll to top