• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.17. Spiritual Food: Weka imani kwa Mungu si mwanadamu

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji wa mtandao huu wa isaack zake. Katika kipengele cha maarifa ya kiroho ya Uliza Neno tunakwenda kujifunza mambo mbalimbali yanayoanishwa na neno la Mungu kwa lengo la kutusaidia utu wetu katika safari na majukumu tuliyonayo hapa duniani siku kwa siku. Katika somo lililopita  tuliendelea kujifunza habari za kusudi la chakula. Makala iliyopita tuliangalia juu ya uweza wa Mungu kutulisha siku zote. Leo tunaangalia juu ya kuweka imani kwa Mungu si kwa mwanadamu. Karibu sana.

 ‘Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa chakula kile cha mbinguni, bali Baba yangu anawapa ninyi chakula cha kweli kitokacho mbinguni’ Yn.6:32

Maneno haya yalisemwa na Bwana Yesu akiwajibu makutano juu ya kauli yao kuhusiana na wazazi wao kula mana kule jangwani kwa mkono wa Musa. Ndipo anawaeleza juu ya kusudi la Mungu kutumia kivuli kile cha agano la kale kwa kuwapa chakula cha kweli kitokacho kwa Bwana Yesu mwenyewe.

Mambo ya kujifunza

  • Wana wa Israel waliweka imani kwa Musa kwamba kupitia yeye walipata chakula. Mtazamo wao ni kuwa Musa aliwawezesha kupata chakula kutoka kwa Mungu. Bwana Yesu anarekebisha mtazamo huu kwa kuwaeleza juu ya chakula hicho kuwa ni Yeye aliyeshuka kutoka mbinguni.

  • Ni muhimu sana kwetu sisi kujifunza katika neno hili ambalo Bwana Yesu anawaambia hawa makutano ya kwamba si Musa aliyewapa chakula cha mbinguni bali Baba anawapa chakula cha kweli. Watu wengi tunawatazama watumishi Fulani na kuwaona wao pekee ndio wana hati miliki ya imani zetu hii si kweli. Mungu anataka tuondoe mitazamo yetu kwa binadamu hata kama anawatumia kutufikishia ujumbe wake au mahitaji yetu bado anabaki kuwa Mungu.

  • Mungu aliweza kutumia kunguru kumlisha Nabii wake mkata wakati wa njaa. Hivyo suala la Mungu kumtumia mtu kukufikishia ujumbe hakubadilishi wala hakupandishi hadhi ya mtu yule kiasi kwamba ukaacha kumsikiliza Mungu.

  • Kamwe hatupaswi kutarajia kupata chakula cha kiroho kutoka kwa mwanadamu bali macho yetu yanapaswa kumtazama Yesu aliye chakula cha kweli kishukacho kila siku kama mana kwa ajili ya kuupa ulimwengu uzima.

  • Lazima tukumbuke hata Musa aliishi kwa mana ile ile waliyokula wana wa Israel, hakuwa na chakula cha tofauti ni sawa na wengine. Hii itupe picha ya kuwa hata watumishi wanaobeba ujumbe kwa ajili yetu bado nao wanategemea chakula hicho hicho ambacho na sisi tunapatiwa.

  • Tafadhali usiweke imani kwa mtu anayetumika kukugawia chakula cha kiroho bali weka imani kwa Mungu anayetupa chakula cha kiroho kupitia watumishi mbalimbali, hii itakusaidia kumwombea mtumishi huyu na itakusaidia na wewe kiasi kwamba hata mtumishi atakapokumbana na changamoto za kiroho na kuteleza au kuanguka imani yako itabaki kuwa imara katika Yesu siku zote.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Isaack Zake ni wakili wa kujitegemea na mshauri katika masuala mbalimbali ya sheria za kazi na rasilimali watu, ndoa na sheria za ardhi na mikataba. Isaack Zake ni mwanzilishi wa mtandao wa kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria wa www.ulizasheria.co.tz ni mwandishi wa vitabu na makala mbalimbali kwenye nyanja za kisheria, kijamii, kiuchumi na kiroho na mwalimu wa makundi mbalimbali ya kijamii kupitia mtandao wa www.isaackzake.co.tz . Isaack Zake pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Uhusiano wa chama cha Waajiri TAACIME – www.taacime.co.tz.

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
May 13, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-05-13 12:46:182020-05-13 12:46:24Day.17. Spiritual Food: Weka imani kwa Mungu si mwanadamu
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Kipaji.4. Kwa nini watu hawawekezi kwenye vipaji vyao? Day.18. Spiritual Food: Je, unapata Chakula cha Kweli?
Scroll to top