• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
SPIRITUAL FOOD

Day.13. Spiritual Food: Imani kwa Yesu na utendaji wa kazi za Mungu

Utangulizi

Karibu sana ndugu yangu msomaji wa mtandao huu wa isaack zake. Katika kipengele cha maarifa ya kiroho ya Uliza Neno tunakwenda kujifunza mambo mbalimbali yanayoanishwa na neno la Mungu kwa lengo la kutusaidia utu wetu katika safari na majukumu tuliyonayo hapa duniani siku kwa siku. Katika somo lililopita  tuliendelea kujifunza habari za kusudi la chakula. Makala iliyopita hii tulijiuliza ‘Unatenda kazi gani ya Mungu?. Leo hii tunazungumzia uhusiano wa imani kwa Yesu na utendaji wa kazi za Mungu. Karibu sana.

 ‘Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndio kazi ya Mungu, mwaminini yeye aliyetumwa na yeye’ Yn.6:29

Maneno haya aliyasema Bwana Yesu ajibu swali la makutano ambalo waliuliza juu ya utendaji wa kazi za Mungu.

Mambo ya kujifunza

  • Tunaona Bwana Yesu akitoa jibu na kuleta tafsiri ya kufanya kazi za Mungu ni kumwamini yeye aliyetumwa na Mungu. Swali muhimu la kujiuliza sisi, je, tunamwamini Bwana Yesu? Kama jibu ni NDIO, je tunaziona kazi za Mungu ndani ya maisha yetu ya kila siku? Je, watu wakitutazama wanaona Mungu akitutumia kama alivyokuwa akimtumia Bwana Yesu?

  • Kila mmoja anafahamu juu ya majibu yake mwenyewe kuhusiana na imani zetu kwa Yesu na endapo tunaziona kazi za Mungu akigusa maisha ya watu wengine kupitia sisi au la.

  • Kama hatuoni sisi wenyewe kazi za Mungu ndani yetu, je, tunamwamini Bwana Yesu ipasavyo? Ni imani ipi hiyo ambayo Bwana Yesu alisema tumwamini yeye aliyetumwa na yeye? Ni imani ya namna gani ambayo Bwana Yesu anaisema inayotuwezesha kufanya kazi za Mungu?

  • Maandiko yanaeleza kwa maneno yake Bwana Yesu kwamba yeye amwaminiye (Bwana Yesu) kazi zile alizozifanya huyo anayemwamini atazifanya pia tena kubwa kuliko hizo. Kama hatuzioni kazi za Mungu ndani ya maisha yetu na kugusa maisha ya watu wengine ni dhahiri imani yetu kwa Bwana Yesu ina upungufu au haijakaa sawa sawa.

  • Ni lazima tutofautishe imani ya kumwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yetu na ile imani ya kutenda kazi pamoja naye. Hizi ni imani tofauti. Watu wengi katika uhusiano wao na Mungu huishia kuokolewa tu hawatafuti zaidi ya hapo, husubiri kifo au unyakuo kwenda Mbinguni. Je, tunamfuata Yesu kwa ajili ya kujihakikishia tiketi ya uzima wa milele kwa sababu tunaogopa Jehanamu? Kama imani yetu imeishia hapa bado tuna changamoto maani inawezekana kabisa baada ya kufika mbinguni na kuwa na uhakika ya kwamba hakuna kwenda jehanamu tunaweza kuachana na Bwana Yesu.

  • Imani ya Bwana Yesu kama Mwokozi au Mponyaji haitoshi kutenda kazi pamoja naye, ni muhimu kuendelea kujifunza zaidi na kupata chakula sahihi cha kiroho ili kuingia ngazi nyingine ya kuzitenda kazi za Mungu katika maisha yetu.

Mungu mwenyewe aliyetuita ni mwaminifu, naye atafanya katika Jina la Mwana wake Mpendwa Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Amen

‘Utupe leo riziki yetu’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Isaack Zake ni wakili wa kujitegemea na mshauri katika masuala mbalimbali ya sheria za kazi na rasilimali watu, ndoa na sheria za ardhi na mikataba. Isaack Zake ni mwanzilishi wa mtandao wa kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria wa www.ulizasheria.co.tz ni mwandishi wa vitabu na makala mbalimbali kwenye nyanja za kisheria, kijamii, kiuchumi na kiroho na mwalimu wa makundi mbalimbali ya kijamii kupitia mtandao wa www.isaackzake.co.tz . Isaack Zake pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Uhusiano wa chama cha Waajiri TAACIME – www.taacime.co.tz.

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho. Mungu akubariki sana.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
April 22, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-04-22 06:23:242020-04-22 06:23:27Day.13. Spiritual Food: Imani kwa Yesu na utendaji wa kazi za Mungu
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Siku ya 6. Mtazamo wa Kiroho kuhusu Corona Virus (Covid – 19) Kipaji.3. Utapimaje kipaji chako?
Scroll to top