• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
ELIMU

AES.19. Upimaji kukosa uhalisia wa utatuzi wa matatizo ya kijamii

Utangulizi

Karibu sana ndugu msomaji wetu. Katika makala zilizopita  tulianza kuzichambua changamoto za mfumo wa elimu katika upimaji, kwa kuangalia kiujumla mojawapo ya changamoto kubwa ya mfumo huu rasmi ya elimu. Katika makala iliyopita tuliangalia  juu ya upimaji unaofanyika katika muda mfupi kuliko upimaji unaopaswa kuwa kwa muda mrefu. Leo tunaangalia juu ya upimaji unaokosa uhalisia wa utatuzi wa matatizo ya kijamii. Karibu sana.

Upimaji wa wanafunzi kitaaluma unategemea sana juu ya kile walichojifunza darasani na si zaidi ya hapo. Taaluma zinafundishwa kupitia mitaala maalum ambayo waalimu wanapaswa kuikamilisha na kuwapima wanafunzi husika kama wameshika kile walichofundishwa.

Hatahivyo, changamoto au matatizo yaliyopo kwenye jamii ni tofauti kabisa na kile kilichopo kwenye mitaala. Hali hii inasababisha nakisi baina ya kinachofundishwa vyuoni na hali ya matatizo kwenye jamii.

Mfumo wa kitaaluma unahitaji uandishi wa tafiti ‘research papers’ ambazo huwasilishwa ili kuwa sehemu ya upimaji wa ufaulu katika taaluma fulani. Hatahivyo, tafiti hizi zimekuwa zikibaki kwenye makabati ya maktaba za vyuo vingi kwa kukosa uhalisia wa utatuzi wa matatizo ya kijamii.

Tukijiuliza kila mmoja wetu aliyeandika tafiti kama anaweza au ameweza kuifanyia kazi kwenye jamii yake, ni watu wachache sana ambao tafiti zao zipo katika utatuzi wa moja kwa moja wa masuala ya kijamii. Kama sisi hatujaweza kuzitumia tafiti tulizofanya katika kuleta suluhu ya kijamii kwenye matatizo ambayo tulianisha katika tafiti maana yake mfumo wetu wa elimu una changamoto ambayo ni kubwa sana na itaendelea kutafuna rasilimali watu wengi zaidi kwenye bara letu la Afrika.

Dunia tunayoenda nayo kwa sasa ipo kasi sana kwenye mabadiliko, hivyo inatupasa upimaji wa kitaaluma utusaidie kupata suluhu za matatizo yanayotukabili kwa sasa.

‘Mungu ibariki Afrika’

Isaack Zake

Wakili, Mwandishi na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
October 17, 2021/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2021-10-17 12:38:182021-10-17 12:38:23AES.19. Upimaji kukosa uhalisia wa utatuzi wa matatizo ya kijamii
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Day.51. Spiritual Food: Si wote ni wateule Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema
Scroll to top