• Twitter
  • Facebook
  • Instagram
Isaack Zake
  • Home
  • Kuhusu Mimi
  • Huduma
  • Vitabu
  • ULIZA
  • Shop
  • Blog
  • Mawasiliano
  • Search
  • Menu Menu
MAANA YA KAZI

Kazi 14. Changamoto za ajira – Hali ya Uchumi

Utangulizi

Karibu tena ndugu msomaji katika mfululizo wa makala hizi za kujifunza juu ya maana ya kazi kwa lengo la kuboresha maisha yetu kila siku na kusaidia watu wengi ambao wanapaswa kufanya kazi ili kuingia kazini.

Katika makala zilizotangulia tumeangalia tofauti za kimsingi baina ya ‘kazi’ na ‘ajira’ambazo zimeelezwa kwa undani zaidi. Sasa tuangalie changamoto zinazokumba sekta ya ajira ili kutuwezesha kubadili mtazamo wetu kutoka katika kutegemea ‘ajira’ na kuanza kufanya ‘kazi’ kwa lengo la kuboresha maisha yetu.

Kama tunavyosema ya kuwa mtu, jamii au taifa halina changamoto ya ukosefu wa ‘kazi’ bali kuna changamoto ya ukosefu wa ‘ajira’ hii ni kwa sababu kila mtu anayo kazi ya kufanya ila si kila mtu ana ajira.

Zipo changamoto kadhaa ambazo zinaikumba sekta ya ajira na kusababisha ongezeko kubwa sana la watu wasio na ajira. Leo tunaangalia changamoto ya kiuchumi.

Hali ya kiuchumi ya mtu binafsi au jamii au taifa au dunia inaweza kwa sehemu kubwa sana kuathiri hali ya kiajira ya eneo au mtu. Kama uchumi wa kijamii au taifa hautakuwa mzuri basi tunatarajia ongezeko kubwa la ukosefu wa ajira. Hivi karibuni tumeshuhudia ongezeko kubwa sana la ukosefu wa ajira kutokana na madhara ya ugonjwa wa Corona ulioikumba dunia yote. Watu wengi wamepoteza ajira zao na zimeendelea kupotea zaidi kwa sababu ya madhara haya.

Hivyobasi, ni muhimu sana kwetu kubadili mtazamo wetu na hasa vijana tunaowaandaa kutokufikiria juu ya ‘ajira’ bali kujifunza juu ya kile kilichopo ndani yao yaani ‘kazi’ ili waweze kuifaa jamii na dunia kwa ujumla. Hii ni kwa sababu suala la uchumi linabadilika mara kwa mara na kuhatarisha ajira za watu lakini mtu mwenye kutenda kazi iliyo ndani yake bado ana uwezo wa kubadilika na kuongeza ufanisi zaidi hata katika hali ngumu za kiuchumi.

Asiyetaka kufanya kazi na asile…’

Isaack Zake

Wakili, Mwalimu na Mshauri

Wasiliana na Isaack Zake kwa barua pepe info@isaackzake.co.tz au kwa simu 0713 888 040 kwa ushauri na mafundisho.

Share this:

  • Click to share on LinkedIn (Opens in new window) LinkedIn
  • Click to share on X (Opens in new window) X
  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
  • Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
November 26, 2020/0 Comments/by Isaack Zake
Share this entry
  • Share on Facebook
  • Share on Twitter
  • Share on WhatsApp
  • Share on LinkedIn
  • Share by Mail
https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png 0 0 Isaack Zake https://isaackzake.co.tz/wp-content/uploads/2020/02/zake-2.png Isaack Zake2020-11-26 20:56:082020-11-26 20:56:11Kazi 14. Changamoto za ajira – Hali ya Uchumi
0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

MAKUNDI YA MAKALA

  • ELIMU (20)
  • FAMILIA (2)
  • KIPAJI CHANGU (14)
  • KUSUDI LA MAISHA (13)
  • MAANA YA KAZI (17)
  • MAKALA (2)
  • NENO LA MUNGU (8)
  • SPIRITUAL FOOD (55)

MAKALA MPYA

  • Day.55. Spiritual Food: Je, ulipo kuna maneno ya uzima wa milele? March 26, 2022
  • Day.54. Spiritual Food: Je, unataka kuondoka? March 24, 2022
  • Day.53. Spiritual Food: Je umekwazwa na kitu gani maishani? January 15, 2022
  • AES.20. Upimaji ni rahisi kuwa na udanganyifu November 8, 2021
  • Day.52. Spiritual Food: Twamwendea Bwana Yesu kwa Neema October 18, 2021

Kuhusu | Vitabu | Mawasiliano

© 2020 Isaack Zake. All Rights Reserved

Kipaji.14. Unaipa nini dunia leo? Kazi 15. Changamoto za ajira – Nafasi
Scroll to top